Kim Jong-un asema wao ni wakosaji,aiomba msamaha Korea Kusini

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un ameomba msamaha kufuatia mauaji ya afisa wa Korea Kusini.

"Komredi Kim Jong-un na Tume ya Maadili hapa kwa moyo wa unyenyekevu, sisi ni wakosaji, tunaomba msamaha wa haya yaliyojitokeza, tumewakosea, tunaomba msamaha," hayo ni kwa mujibu wa maelezo yaliyonukuliwa kutoka Jamhuri ya Watu wa Korea.
Kufuatia tukio hilo la Ijumaa, Kim ameripotiwa kumwambia mwenzake wa Korea Kusini Moon Jae-in kwamba, tukio hilo halikustahili kufanyika, hivyo wanaomba msamaha.

Korea Kusini inadai mtu huyo mwenye umri wa miaka 47 alikuwa akijaribu kutoroka kutoka Korea Kaskazini alipopatikana na wanajeshi wa nchi hiyo ambao walikuwa wakishika doria ambapo alipigwa risasi na mwili wake kuteketezwa moto.

Hayo yanajiri wakati mpaka kati ya Korea hizo mbili unalindwa vikali na Kaskazini inadaiwa kutekeleza sera ya kuua kwa kupiga risasi ili kumzuia mtu huyo asiingize virusi vya corona (COVID-19) nchini humo.

Msamaha huo ulitolewa kupitia njia ya barua iliyotumiwa Rais Moon kuelezea kuwa tukio hilo halikustahili kufanyika, kwa mujibu wa afisa mmoja nchini humo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news