Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya ACT Wazalendo,Maalim Seif Sharif Hamad akiulizia bei ya Muhogo katika soko la Mikunguni Mjni Unguja ambapo alifanya ziara maalumu kusikiliza kero kwa watumiaji wa soko hilo mapeema leo asubuhi Septemba 26,2020, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Jambo kubwa ambalo amesisitiza ni kwamba iwapo watamchagua Oktoba 28, mwaka huu kuwa Rais wa Zanzibar atahakikisha wakulima na wafanyabiashara wanafurahia kazi zao.
Amesema, atafanya hivyo kwa kuwawekea mazingira wezeshi ambayo yatampa fursa kila mmoja kunufaika zaidi.