Mhandisi Kemikimba:Matokeo ya kazi yetu ni wananchi kupata huduma ya maji

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba amewataka watendaji katika sekta ya maji nchini kuhakikisha matokeo ya kazi zao ni wananchi kupata huduma ya maji ya uhakika, anaripoti Happiness Shayo (WM).

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba (katikati) akifungua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wawezeshaji watakaozijengea uwezo bodi za wakurugenzi wa mamlaka za maji nchini katika masuala ya menejimenti. Mafunzo yamefanyika katika ukumbi wa DUWASA jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji, Mhandisi Charles Mafie na Mwezeshaji Mhandisi Alex Kaaya (kushoto).

Mhandisi Kemikimba amesema hayo leo Septemba 24, 2020  jijini Dodoma wakati akishiriki mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wawezeshaji wa sekta ya maji atakaofanya kazi ya kuzijengea uwezo bodi za wakurugenzi wa mamlaka za maji hasa katika menejimenti ya mamlaka hizo.

Mkurugenzi wa Usambazaji Maji, Mhandisi Charles Mafie akiongea na wataalam wa sekta ya maji kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba (kushoto) kufungua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wawezeshaji wa Sekta ya Maji yaliyofanyika ukumbi wa DUWASA jijini Dodoma leo.

“Mhakikishe mafunzo mtakayoyatoa kwa bodi za wakurugenzi wa mamlaka za maji nchini yanasaidia kufikia malengo ya sekta yetu ya maji na ya kitaifa kwa kuwapatia wananchi huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza,”Mhandisi Kemikimba amesema.

Mwezeshaji Mhandisi Alex Kaaya akitoa mafunzo kuhusu menejimenti hususan katika mamlaka za maji nchini ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, amewashauri washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia suala la ufuatiliaji na tathmini katika ufundishaji wao ili hatimaye Serikali iweze kujua huduma ya maji kwa wananchi inapatikana kwa kiwango gani katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mhandisi Kemikimba amesema, kuongea lugha moja katika huduma ya maji ni jambo la msingi, hivyo ni muhimu kujua wananchi wanapokeaje huduma hiyo na mrejesho wao unafanyiwa kazi kwa haraka.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba (katikati) katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa Sekta ya Maji baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika ukumbi wa DUWASA jijini Dodoma leo.

Mamlaka za maji ni matokeo ya mabadiliko yaliyofanywa na serikali miaka ya 90 ambapo zilikasimiwa madaraka ili kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa wananchi

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news