"Tunaomba kura zenu ili biashara zitoke na wananchi waweze kufanya biashara, uwekezaji uongezeke, vitunguu vipate soko sio tu Tanzania mpaka Afrika Mashariki yote, watu wapewe utaalamu wa kuweza kuongeza tija katika shughuli zao za kilimo.
"Maana mkiwapa CCM miaka mitano mingine, hivyo vyuma si ndiyo vitatumaliza kabisa, kama hivi sasa vijana wa Ilula mnazeeka kabla ya wakati wenu unaweza ukaja hapa ukamwamkia mtu shikamoo kumbe ni kijana wa juzi bakora za CCM zimemchanganya, kila mtu yupo hoi bin taabani na ndugu zangu bakora za CCM hazina ubaguzi;
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ambaye ni mgombea urais kupitia CUF ameyasema hayo Septemba 13, mwaka huu wakati akiendelea na kampeni zake za kuomba wananchi ifikapo Oktoba 28, mwaka huu wampe kura kwa nafasi ya urais, kuchagua wabunge wa CUF na madiwani ili wakawape furaha.
Ameyasema hayo katika mwendelezo wa kampeni zake mkoani Iringa huku akisisitiza kuwa, CUF ikipewa ridhaa wameazimia kuwekeza katika rasilimali watu, elimu, afya na miradi mbalimbali ambayo itawakwamua wananchi katika umaskini.
Pia amesisitiza kuwa,wakipewa ridhaa watauenzi Muungano uliopo kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwani ni nguzo muhimu kwa Taifa na haki sawa itapewa nafasi kwa pande zote.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa Serikali yake itakipa umuhimu mkubwa kilimo kutokana na faida zake kwa jamii na Taifa, kwani kiunasaidia upatikanaji wa malighafi za viwandani ambazo zina umuhimu mkubwa katika kukuza uchumi.
Mgombea Urais kupitia CUF, Profesa Ibrahim Lipumba |
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ambaye ni mgombea urais kupitia CUF ameyasema hayo Septemba 13, mwaka huu wakati akiendelea na kampeni zake za kuomba wananchi ifikapo Oktoba 28, mwaka huu wampe kura kwa nafasi ya urais, kuchagua wabunge wa CUF na madiwani ili wakawape furaha.
Ameyasema hayo katika mwendelezo wa kampeni zake mkoani Iringa huku akisisitiza kuwa, CUF ikipewa ridhaa wameazimia kuwekeza katika rasilimali watu, elimu, afya na miradi mbalimbali ambayo itawakwamua wananchi katika umaskini.
Pia amesisitiza kuwa,wakipewa ridhaa watauenzi Muungano uliopo kati ya Tanzania Bara na Zanzibar kwani ni nguzo muhimu kwa Taifa na haki sawa itapewa nafasi kwa pande zote.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa Serikali yake itakipa umuhimu mkubwa kilimo kutokana na faida zake kwa jamii na Taifa, kwani kiunasaidia upatikanaji wa malighafi za viwandani ambazo zina umuhimu mkubwa katika kukuza uchumi.