Skuli ya Sekondari Lumumba yafanyiwa maboresho ya kisasa

Jumla ya shilingi bilioni 1.79 zimetumika kwa ajili ya kufanya matengenezo Skuli ya Sekondari ya Lumumba ili kuirejesha katika hadhi yake,anaripoti Talib Ussi (Diramakini) Zanzibar.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya Skuli ya Sekondari Lumumba baada ya kumaliza kufanyiwa matengenezo, Mkurugenzi wa Idara ya Mipango Sera na Utafiti Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bw.Khalid Masoud Waziri amesema wizara hiyo imekuwa ikifanya matengenezo majengo yake kila mwaka kupitia ruzuku ya bajeti yake kutoka serikalini ili kuimarisha skuli zake na kutoa kiwango bora cha elimu.
Bw.Khalid amesema, matengenezo hayo yamefanyika kwa skuli yote kwa kuondoa bati zote na kuezeka bati mpya ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba mpya ya walimu ili kuweka walimu karibu na skuli waweze kutoa elimu kwa wanafunzi kwa ufanisi zaidi.

Amesema kuwa, matengenezo hayo makubwa yamejumuisha maabara zote za Kemia,Biolojia na Fizikia, maktaba, madarasa ya kusomea, ofisi, nyumba ya walimu pamoja na ukumbi wa kufanyia mitihani.

Akizungumza baada ya kusaini makabidhiano ya skuli hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar,Mhandisi Idrissa Muslim Hija amesema, wizara yake imeanza kurekebisha baadhi ya majengo yaliochakaa ili kuendelea kuimarisha sekta ya elimu na miundombinu yake.

Dkt Idrisa amesema ukarabati wa skuli hiyo utasaidia kuimarika utoaji wa elimu katika mazingira bora kwa wanafunzi na kuwafanya kupata haki yao ya elimu katika mazingira mazuri na salama.

Amesema,ushirikiano mzuri uliopo kati ya wakandarasi wa skuli hiyo pamoja na wakandarasi wa Wizara ya Elimu Zanzibar umepelekea kuifanya kazi hiyo katika ubora.

Kwa upande wake Mhandisi  Mkuu wa Kampuni ya Modern Building Contractor Ltd, Ali Pandu Sharif  amesema wamehakikisha wanafanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wanamaliza matengenezo hayo ingawa kulijitokeza tatizo, lakini kwa ushirikiano wao mzuri na wizara tatizo hilo waliweza kulimaliza.

Ukarabati wa skuli ya Sekondari Lumumba ulianza rasmi Januari 3, mwaka huu na kumalizika Septemba 19,2020.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news