Tetesi:Kurt Zouma,Sergino Dest,Mickael Cuisance,Andreas Pereira wanasakwa

Manchester United itamruhusu winga raia wa Wales Daniel James, kujiunga na Leeds United kwa mkopo, lakini kama watamsajili Sancho hiyo ikiwa ni kwa mujibu wa Sun. Huku Everton na Leicester City zote zinamnyatia mlinzi wa Chelsea raia wa Ufaransa Kurt Zouma (25) hayo yakiwa ni kwa mujibu wa Talk Sport.

Kurt Zouma. (GettyImages).
Nao Sheffield United kwa mujibu wa Sun imetoa ofa kwa Liverpool ya pauni milioni 17 kwa mshambuliaji wa England wa Under (21), Rhian Brewster na iko tayari kujumuisha kipengele cha kumnunua kwenye makubaliano.

Aidha, Barcelona kwa mujibu wa Goal, inakaribia kufikia makubaliano ya mwisho na Ajax kuhusu beki wa kulia wa Marekani Sergino Dest (19), lakini ina uwezo mdogo wa kufanya makubaliano zaidi ya usajili. Cope inaeleza kuwa,mlinzi wa Tottenham na Argentina Juan Foyth (22) ndiye mlengwa wa Valencia.

Leeds United iko katika hatua ya mwisho ya majadiliano na Bayern Munich kuhusu kiungo wa kati Mickael Cuisance (21), baada ya raia huyo wa Ufaransa kuiarifu klabu yake ya Ujerumani kuwa anataka kuingia kwenye kikosi cha wachezaji mara kwa mara, hii ikiwa ni kwa mujibu wa Sport Bible.

Sky Sports wanasema, Lyon ipo tayari kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa, Houssem Aouar (22) ambaye anahusishwa na kuhamia Arsenal. 

Kwa upande wa Mail wanaeleza kuwa, kocha wa Everton Carlo Ancelotti hatarajii kuwa winga Theo Walcott (31),ataondoka katika klabu hiyo kipindi hiki cha usajili.

Wakati huo huo, Lazio inafanya mazungumzo kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United raia wa Brazil Andreas Pereira (24), kwa kipindi kirefu kwa mkopo kukiwa na chaguo la kumnunua,Telegraph imeeleza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news