Thiago Silva:Ninajisikia furaha sana kuwa hapa

Thiago Silva ambaye ni mlinzi wa Chelsea anasema hana wasiwasi na kasi ya Ligi ya Premier licha ya kutimiza miaka 36 siku moja kabla ya kujitokeza katika klabu hiyo.
Mlinzi wa Chelsea, Thiago Silva. (Diramakini).

Beki huyo wa kati wa Brazil aliungana na Frank Lampard wa Blues kwa uhamisho wa bure mwezi uliopita, baada ya kushinda mataji saba ya Ligi akiwa na Paris St.Germain.

Silva atacheza katika mechi ya Jumatano kwenye raundi ya tatu ya Kombe la Carabao wakiwa nyumbani dhidi ya Barnsley."Umri ni namba tu kwenye stakabadhi yako. Sina wasiwasi kabisa kuhusu kasi ya Ligi ya Premier.

"Kimwili, najihisi kijana na nimejitayarisha vilivyo kwa hili. Pia najisikia furaha sana kuwa hapa. Watu wanaonijua, wanafahamu ni kiwango gani ninapenda kazi yangu, vile ninavyojitahidi kuweka nguvu yangu kwa asilimia 200. Hii ni fursa nzuri ambayo Chelsea na Frank Lampard wamenipa na sitaki kuwakatisha tamaa,"amesema.

"Nakuja hapa kama mchezaji mzoefu, na hivyo basi naona vile Chelsea na Frank Lampard wanavyotaka mchezaji mwenye tajriba kama yangu," Silva aliongeza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news