Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), upepo wa Pwani unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya kilomita 30 kwa saa kwa Pwani yote kutoka Kusini Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini na kutoka Mashariki kwa Pwani ya Kusini, vivyo hivyo hali ya bahari inatarajiwa kuwa na mawimbi makubwa kiasi.Pia meneo mengi yanatarajiwa kuwa na mawingu kiasi na vipindi vya jua. TMA inabainisha kuwa, matarajio kwa siku ya Alhamisi ya Septemba 17, 2020 kutakuwa na mabadiliko kidogo.
|