Mbwana Samatta afanya kweli huko Uturuki

Hatimaye Nahodha wa Timu ya Taifa (Taifa Stars), Mbwana Samatta amewathibitishia wote kwamba ana kipaji zaidi ya wanavyomuuona.

Ni baada ya leo Oktoba 3,2020 kuifungia mabao mawili timu yake ya Fenerbahce katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Karagümrük kwenye Ligi Kuu nchini Uturuki.
Aidha, hii ni mechi ya pili kwa Mbwana Samatta kwenye ligi hiyo ambapo amecheza kwa 84' kabla ya mabadiliko.

Hata hivyo, mechi yake ya kwanza ilikuwa ni dhidi ya Galatasaray wiki iliyopita ambapo alicheza kwa dakika 25 huku mechi ikimalizika kwa suluhu nchini humo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news