NEC yavikabidhi vyama vya siasa nakala tepe ya Daftari

 Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) imekabidhi kwa vyama vya siasa nakala tepe ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Sambamba na orodha ya vituo vya kupigia kura, mfano wa karatasi ya kupigia kura kwa nafasi ya kiti cha Rais na Makamu wa Rais na jalada la nukta nundu (tactile ballot folder), anaripoti Mwandishi Diramakini.

Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dkt.Wilson Mahera Charles amesema, makabidhiano hayo ya leo Oktoba 15,2020 yanafanyika kwa mujibu wa Kanuni ya 37 ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura za mwaka 2018 ambayo inaielekeza tume kuvipatia vyama vya siasa nakala ya daftari kwa ajili ya utambuzi wa wapiga kura wanaoingia katika kituo cha kupigia kura.

Dkt.Charles amesema kuwa, orodha ya kupigia kura imetolewa kwa vyama vya siasa ili kuviwezesha vyama kuwasilisha orodha ya majina ya mawakala watakaopangwa katika vituo hivyo siku ya kupiga kura.

"Vyama vya siasa vinashauriwa kutumia mfano wa karatasi ya kura ambazo zimetolewa kwa vyama vya siasa kuwaelimisha wanachama na wafuasi wao kupiga kura kwa usahihi ili kupunguza idadi ya kura zinazoharibika.

"Kwa kuwa zimebaki siku 12 kufikia tarehe 28 Oktoba, 2020 ambayo ni siku ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani. Tume inavitaka vyama vya siasa na wagombea kuendelea kuzingatia maadili ya uchaguzi, kunadi sera na kuwahimiza wafuasi wao kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani,"amefafanua Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dkt. Wilson Mahera Charles.Video tazama hapa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news