Oktoba 3, 2020 imeondoka namna hii!


Septemba 22, mwaka huu Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo , Zitto Kabwe amesema vyama vya upinzani nchini vimekubaliana kumuunga mkono Mgombea mmoja wa Urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania na pia, kwa upande wa Zanzibar.

Zitto ameongeza kuwa Oktoba 3, 2020 watatangaza ni nani hasa atasimama kama Mgombea Urais katika mkutano wa hadhara utakaohusisa CHADEMA, ACT Wazalendo na vyama vingine vya upinzani.

Amesema ACT-Wazalendo wameshajadiliana na wameshawasilisha mapendekezo yao kwa CHADEMA na baada ya pande zote kukamilisha mazungumzo watatangaza makubaliano yatakayofikiwa.

Ameripoti Mwandishi Diramakini (diramakini@gmail.com).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

1 Comments

Previous Post Next Post

International news