Rais Trump, mke wake Melania wathibitika kuwa na Corona

Rais wa Marekani, Donald Trump na mke wake Melania Trump wamethibitka kuwa wameambukizwa virusi vya Corona (Covid-19), anaripoti Mwandishi Diramakini.

Matokeo hayo yanakuja siku moja baada ya mshauri wake wa karibu kuthibitika ana COVID-19 baada ya kusafiri naye kupitia ndege ya Air Force One.

"Hope Hicks, ambaye amekuwa akitimiza majukumu yake bila kuchoka na bila kupumzika hata kidogo, amegundulika ana maambukizi ya Covid-19.Ni tatizo, Mke wangu na Mimi tunasubiria matokeo ya vipimo, hivyo muda wowote tutaanza mchakato wa kukaa karantini,"amesema awali Rais Trump kupitia ukuta wake wa Twitter kabla ya matokeo ya sasa ambayo yamethibitisha rasmi Covid-19.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news