TAARIFA ZA AWALI,MAZISHI YA MZEE WA IMANI REV. WILSON KIMARO

 "Tunamtaka Bwana na Nguvu zake. Taarifa za awali za mazishi ya Mzee wetu wa Imani Rev. Wilson Kimaro ni kama ifuatavyo:

1. Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano tarehe 7 Oktoba 2020 huko Arusha. 


2. Familia inaendelea kufuatilia kibali ili iliwezekana Mpendwa wetu azikwe kwenye eneo la makazi/nyumbani kwake Ngaramtoni.

3. Shughuli zote za Ibada ya Mazishi (kuaga, rambirambi nk) zitafanyikia TAG Calvary Temple - Arusha ili kuruhusu tu watu wachache kwenda eneo la mazishi kwa sababu ya ufinyu wa eneo hilo.

4. Ratiba kamili ya Shughuli nzima ya siku hiyo ya Jumatano itafuata hapo baadae.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake libarikiwe. 

Rev. Dr. Boniface Mgonja

KATIBU MKUU

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news