Wanafunzi wakiri mbele ya polisi kujihusisha na wizi vifaa vya shule

Jeshi la Polisi mkoani Tabora linawashikilia wanafunzi watatu kwa tuhuma za kujihusisha na wizi wa vifaa vya ujenzi wa shule, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Tabora, Barnabas Mwakalukwa amesema kuwa, tukio hilo limetokea majira ya saa 12 jioni ya Oktoba 15, mwaka huu katika Kijiji cha Manoleo Kata ya Itonjanda  iliyopo Manispaa ya Tabora.

Amesema, wanafunzi hao ni wa Shule ya Sekondari Itonjanda ambao wanakabiliwa na tuhuma za kuiba mifuko minne ya saruji,viti vitano na nondo tano zote mali ya Shule ya Msingi Manoleo ambapo baada ya kubanwa wamekiri kutenda hivyo na hatua zaidi zitachukuliwa.

Kamanda amesema kuwa, majira hayo walimkamata Hasani haruna (18) mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari ya Itonjanda na wenzake wawili ambao ni wanafunzi wakiwa na vitu hivyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news