LIVE:Simba SC vs Platinum Desemba 23, 2020

Simba SC walifanikiwa kuingia Hatua ya 32 Bora michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya sare ya 0-0 na Plateau United ya Nigeria katika mchezo wa marudiano Raundi ya Awali hivi karibuni Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Kwa matokeo hayo, Simba SC ilisonga mbele kwa ushindi wa 1-0 ulioupata kutokana na bao pekee la Mzambia, Clatous Chama kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Kimataifa wa Jos, Nigeria.

Leo Wekundu wa Msimbazi wanamenyana na Platinum FC ya Zimbabwe iliyoitoa Costa do Sol ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 4-1 ikishinda 2-1 ugenini na 2-0 mjini Bulawayo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news