
Amesema hayo leo Desemba 2, 2020 wakati wa kukusanya mawe kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala katika shule mpya ya Sekondari ya Kata ya Igulwa ambayo inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi mwezi Januari,mwakani.
Shule hiyo ina vyumba vya madarasa vilivyokamilika vitano ambavyo vilijengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na Mbunge huyo kuchangia mabati yote,saruji mifuko 300 na fedha za mafundi ujenzi.
Mbunge huyo amesema kuwa, Wilaya ya Bukombe ambayo ndiyo jimbo la uchaguzi haikuwa na shule ya kidato cha tano, lakini baada ya kuomba kibali kutoka serikalini kupandisha hadhi shule mbili za sekondari, serikali imewapatia milioni 500 za kuboresha miundombinu ya shule hizo na muda wowote zinaanza kupokea wanafunzi.
Ameongeza kuwa,anatamani wanafunzi wengine wa kutoka mikoa mingine waje kusoma Bukombe na wanafunzi wa Bukombe wapangiwe kusomea mikoa mingine ili kujenga utaifa kwa kuchangamana na kushirikishana mambo mbalimbali kama mila na desturi zetu.
Pia amesema, baadhi ya wanafunzi wanashindwa kwenda shule kwa sababu ya kipato hafifu cha familia zao hasa kukosa nauli,hivyo ujenzi wa shule hizo maeneo ya karibu utasaidia hata wanafunzi wanaotoka familia hizo kupata elimu kwa urahisi bila kulazimika kusafiri kwenda mbali au mikoa mingine.
0 Comments