Mtandao wa wizi wa magari wanaswa Njombe

Jeshi la polisi mkoani Njombe linawashikilia watu watano wanaodaiwa kuhusika na mtandao wa wizi wa magari nchini ambao wamekutwa na magari Saba yanayosadikiwa kuibwa katika mikoa ya Dar es salaam, Mbeya na Singida.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Njombe, - Hamis Issah amesema wezi hao wamekuwa wakiiba magari na kuyabadilisha rangi na kubadili namba za injini.

Kamanda Issah amewataja Watuhumiwa hao wa wizi wa magari kuwa ni Edrick Hussein maarufu kwa jina la Kimya Kimya mkazi wa jijini Dar es salaam, Sudi Abuba Mwinyi mkazi wa Uyole Mbeya, Method Mkongwa mkazi wa Njombe, Imani Fidelis mkazi wa Moshi Kilimanjaro na Timoth Nehemia mkazi wa Mufindi.

Watuhumiwa hao pia wamekutwa na vifaa mbalimbali vya magari na ufundi wa magari vinavyodhaniwa kutumika katika wizi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news