Mtoto wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere afariki

Januari Mosi, 2021 familia ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere imepata msiba wa mtoto wao, Rosemary Nyerere aliyefariki jioni jijini Dar es Salaam, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Rosemary Nyerere enzi za uhai wake.
Wanafamilia akiwemo Sophia Nyerere na Manyerere Jacton wamethibitisha kifo cha Rosemary Nyerere huku Sophia Nyerere akiandika katika mtandao wa Instagram kuwa shangazi yake amefariki.  

Taarifa zaidi kuhusu msiba zitatolewa hapo baadaye na Familia ya Marehemu. Rosemary ni miongoni mwa watoto saba wa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news