MWALIMU ATIWA HATIANI KWA KOSA LA KUHUJUMU UCHUMI

Ofisi ya TAKUKURU mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashitaka, imemfikisha katika mahakama ya wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Mwalimu Wilfred Emanuel Manumbu kwa makosa ya mawili, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Kosa la kwanza ni wizi akiwa mtumishi wa umma ambapo anatuhumiwa kumwibia mwajiri wake ambaye ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kiasi cha sh. 10,947,400/= na kosa la pili ni kumsababishia hasara mwajiri wake ambaye ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kiasi cha sh. 10,947,400/=.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na H.M MUSSA, Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga.

Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 07/2021 mshtakiwa alikiri kutenda makosa hayo ambayo aliyafanya kati ya mwezi Oktoba 2013 na Januari 2016 huko katika Halmashauri ya wilaya ya Ushetu alikokuwa ameajiriwa kama Mwalimu wa Shule ya Msingi Nyaweshi.

Mshtakiwa alikiri makosa yake na mahakama imemtia hatiani kwa makosa yote mawili na kumhukumu kwenda jela miaka mitatu (03) na kulipa fedha zote alizohujumu kiasi cha sh. 10,947,400/=

Natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuendelea kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU ili kuhakikisha kuwa tunaondoa kero za rushwa katika mkoa wetu wa Shinyanga.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news