Utabiri wa hali ya hewa/ Weather Forecast today February 20th, 2021

 

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO KUANZIA SAA 3.00 USIKU WA LEO:
TAREHE: 20/02/2021.

Mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya na Songwe: Inatarajiwa kuwa na Hali ya mawingu, mvua na ngurumo katika baadhi ya maeneo na vipindi vifupi vya jua.
..........
Mikoa ya Lindi na Mtwara: Hali ya mawingu, mvua na ngurumo katika maeneo machache na vipindi vifupi vya jua.
........
Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Tabora, Iringa, Njombe, Dar es salaam, Tanga, Pwani ( ikijumuisha Visiwa vya Mafia), Visiwa vya Unguja na Pemba: Hali ya mawingu kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache na vipindi vya jua.
.........
Mikoa ya Manyara, Kilimanjaro, Arusha Dodoma, Singida, Ruvuma na Morogoro: Inatarajiwa kuwa na Hali ya mawingu kiasi, mvua katika maeneo machache na vipindi vya jua.
..........
VIWANGO VYA JOTO, VYA JUA KWA BAADHI YA MIJI HAPA NCHINI:
MJI                   Kiwango cha juu  Kiwango chachini 
                         cha joto               cha joto
ARUSHA            27°C                   15°C 
D'SALAAM        31°C                    25°C 
DODOMA          30°C                   20°C 
KIGOMA            26°C                   21°C 
MBEYA               27°C                  16°C 
IRINGA              28°C                   17°C 
NJOMBE            21°C                   13°C 
MWANZA          26°C                   22°C 
TABORA             28°C                   19°C 
TANGA               32°C                   24°C 
ZANZIBAR          31°C                   24°C
..........
Upepo wa Pwani: Unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya km 30 kwa saa kutoka Kaskazini Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini; na kwa kasi ya km20 kwa saa kutoka Kaskazini kwa Pwani ya Kusini.

Hali ya Bahari: Inatarajiwa kuwa na Mawimbi Madogo hadi makubwa kiasi.
Matarajio kwa siku ya Jumatatu tarehe 22/02/2021: Kuongezeka kwa mvua.
Utabiri huu umetolewa leo tarehe: 20/02/2021.
Na: MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.


MATARAJIO YA HALI MBAYA YA HEWA KWA SIKU TANO ZIJAZO.

..........

Jumamosi 20-02-2021

HAKUNA TAHADHARI

..........

Jumapili 21-02-2021

HAKUNA TAHADHARI 

.........

Jumatatu 22-02-2021 

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa

baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha,Kilimanjaro, Manyara, Dar es Salaam,Pwani (ikijumuisha Visiwa vya Mafia),Kaskazini mwa Morogoro, Lindi na Mtwara pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba

UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI

KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA: WASTANI 

Athari zinazoweza kujitokeza: Baadhi ya makazi kuzungukwa na maji pamoja na ucheleweshwaji wa baadhi ya shughuli za usafirishaji.

Tafadhali zingatia na ujiandae.

...........

Jumanne 23-02-2021

ANGALIZO la mvua kubwa limetolewa kwa

baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha,Kilimanjaro, Manyara, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha Visiwa vya Mafia), Morogoro, Ruvuma, Lindi na Mtwara pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba.

UWEZEKANO WA KUTOKEA: WASTANI

KIWANGO CHA ATHARI ZINAZOWEZA KUTOKEA:WASTANI

Athari zinazoweza kujitokeza: Baadhi ya makazi kuzungukwa na maji pamoja na ucheleweshwaji wa baadhi ya shughuli za usafirishaji.

Tafadhali zingatia na ujiandae.


Jumatano 24-02-2021

HAKUNA ANGALIZO


Imetolewa leo tarehe 20/02/2021

Na. MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news