Waziri Nchemba:Wanaozusha taarifa za vifo washughulikiwe haraka

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza vyombo husika kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaosambaza taarifa za uongo mitandaoni kuhusu afya za watu wengine, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Mheshimiwa Dkt. Nchemba amesema hayo kufuatia uwepo wa uvumi mwingi mitandaoni kuhusu hali za afya za watu mbalimbali huku akifafanua kwamba, kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao kinazuia watu kutoa taarifa za uongo.

"Kumetokea tabia mbaya ya kuzushiana, (na fulani anaumwa, na fulani naye anaumwa. Mara nasikia fulani amekufa na fulani naye amekufa). Huku ni kukosa utu, ni kuathiri maisha binafsi ya mtu, familia yake na kusababisha taharuki kwenye jamii.

"Nimeelekeza vyombo vyote husika kuchukua hatua bila kusubiri mtu binafsi akalalamike," amesema Waziri Dkt.Nchemba huku akiwataka wananchi kuacha tabia hiyo mara moja.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news