Anuary Jabir,Zubery Katwila,John Nzwalla watwaa tuzo ya mwezi Februari Ligi Kuu ya Tanzania Bara

Kijana Anuary Jabir ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa mwezi Februari, 2021 huku Kocha wa Ihefu SC, Zubery Katwila akishinda tuzo ya Kocha Bora wa Ligi Kuu kwa mwezi huo, anaripoti Mwandishi DIRAMAKINI.

Katika hatua nyingine John Nzwalla ambaye ni Meneja wa Uwanja Nelson Mandela uliopo Sumbawanga mkoani Rukwa ameshinda tuzo ya Meneja Bora wa Uwanja wa mwezi Februari, mwaka huu.
Kwa sasa Anuary Jabir amekuwa gumzo kutokana na kasi yake ya upachikaji mabao katika msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mabao saba aliyofunga kwenye mechi nne alizocheza kuanzia raundi ya pili ikiwa zote alifunga katika mechi dhidi ya JKT Tanzania, Coastal Union, Polisi Tanzania na Kipigwe FC na kumfanya afikishe idadi hiyo ndani ya mechi nne.

Ukiachana na mabao matatu aliyonayo kwenye Kombe la Shirikisho, Anuary hivi sasa ana mabao manne huku akiweka lengo la kufunga zaidi mabao kwenye mechi zijazo hadi awafikie wanaoongoza kwa ufungaji Ligi Kuu Tanzania Bara.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news