Machi 28 ngumu; Wakurugenzi nane kikaangoni kufuatia agizo la Rais Samia


Wakurugenzi nane ambao Halmashauri zao zimepata Hati Chafu majina yao kuwasilishwa katika Mamlaka ya Uteuzi kwa hatua zaidi,anaripoti Mwandishi DIRAMAKINI.

Akizungumza na Waandishi wa habari Habari Jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo, amesema atawasilisha majina ya Wakurugenzi hao kwenye Mamlaka yao Uteuzi kwa ajili ya hatua stahiki.
 
"Kwakuwa Wakurugenzi wa Halmashauri Mamlaka yao ya Uteuzi ni Mhe. Rais, nitawasilisha majina yao ili wachukuliwe hatua kwa kadiri atakavyoona inafaa‘ amesema Jafo.

Wakati huo huo Waziri Jafo amewataka watendaji wote katika Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuendelea kuchapa kazi kwa uadilifu katika kuwatumikia wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news