🔴𝐋𝐈𝐕𝐄:Maelfu ya Watanzania wanauaga mwili wa Hayati Dkt. Magufuli katika Uwanja wa Uhuru

 Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, tangu kuchaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2015 alijipambanua kama mtu wa vitendo, tofauti na watangulizi wake.

Namna yake ya kutekeleza majukumu ikiwemo kutumbua majipu ilimpatia mashabiki wengi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania hususan katika Ukanda wa Afrika Mashariki ambako kampeni ya #WhatWouldMagufuliDo iliibuka na kupata umaarufu kwa kusifia utendaji wake usiokuwa na simile katika mapambano dhidi ya ufisadi na kusimamia miradi ya ujenzi wa miundo mbinu bila kuchoka. 

Watanzania walizingatia zaidi mtindo mashuhuri wa uongozi wa Magufuli ambao ulikuwa mfano wa kusifiwa na viongozi wengine Barani Afrika.

Kipenzi cha watu

Wafuasi wake watakosa mikutano yake ya mara kwa mara alipokuwa ziarani katika maeneo mbalimbali ambapo alisimama mara kadhaa vituoni kuzungumza na wananchi.

Ziara hizo ambazo mara nyingi ziliibua udhaifu wa watendaji wa serikali zilitangazwa mubashara katika runinga na kupata umaarufu kwa wananchi wengi kutumia fursa hiyo kuelezea matatizo yao huku yakipatiwa ufumbuzi papo kwa papo. BURIHANI SHUJAA WA WATANZANIA HAYATI DKT.MAGUFULI.

 RATIBA YA KUAGA MWILI WA JPM

Machi 20- Mwili kupelekwa Uwanja wa Uhuru kwa taratibu za kuaga
Machi 21- Dar es Salaam
Machi 22- Dodoma
Machi 23- Zanzibar
Machi 24- Mwanza
Machi 25- Familia na wakazi wa Geita
Machi 26- Mazishi mkoani Geita.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news