BALOZI LIBERATA MULAMULA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA, UFARANSA, ISRAEL, UBELGIJI NA UJERUMANI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mhe.Frederick Clavier mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masharika Jijini Dodoma. Mazungumzo hayo yalilenga kudumisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili katika Nyanja za diplomasia ya mahusiano na uchumi,biashara na uwekezaji
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Israel hapa Nchini Balozi Oded Joseph mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dodoma. Katika mazungumzo hayo Balozi Mulamula amemsihi Balozi Oded kuhakikisha Israel inakuwa na Ubalozi wake rasmi hapa Nchini na kumshukuru kwa hatua ya Israel kuwachukuwa vijana wa Kitanzania kwenda Nchini humo kwa mafunzo ya vitendo na nadharia kuhusu kilimo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Ubelgiji hapa Nchini Balozi Peter Van Acker mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dodoma. Mazungumzo hayo yalilenga pamoja na mambo mengine ukamilishwaji wa majadiliano ya ushirikiano katika sekta ya usafiri wa anga na kuimarisha ushirikiano katika sekta za kilimo na usambazaji wa maji safi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi Regina Hess mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dodoma. Pamoja na masuala mengine Viongozi hao walijadili masuala ya ushirikiano katika sekta ya afya,elimu,biashara,uwekezaji pamoja na maliasili na utalii.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Mb) Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi wa China hapa Nchini Balozi Wang Ke. Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha mahusiano baina ya Nchi hizo katika nyanja za kiuchumi,kibiashara na uwekezaji ambapo moja ya suala walilolijadili ni kuanza kwa safari za ndege (ATCL) kwenda Guangzhou Nchini China mara moja kila baada ya wiki mbili.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news