BAKWATA yatangaza Sikukuu ya Eid Ijumaa ya Mei 14, 2021

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Ally amesema hakuna taarifa za kuandama kwa mwezi leo na hivyo Waislamu wataendelea kufunga na kujiandaa na Sikukuu ya Eid Ijumaa ya Mei 14, 2021, anaripoti Mwandishi Diramakini.
Sherehe za Eid El- fitr kitaifa kwa mwaka huu zitafanyika Mkoa wa Dar es Salaam, swala ya Eid itaswaliwa katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 1:30 asubuhi.

Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limesema Baraza la Eid litafanyika katika viwanja vya Karimjee kuanzia saa 8:00 mchana.

Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news