WATUMISHI WILAYANI ILEJE NA MOMBA WATAKIWA KUWA WAADILIFU ILI KUTEKELEZA AZMA YA RAIS YA KUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Na James K. Mwanamyoto, Songwe

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amewataka Watumishi wa Umma wa Halmashauri za Wilaya ya Ileje na Momba mkoani Songwe kuwa waadilifu mahala pa kazi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kuujenga Utumishi wa Umma kuwa unaozingatia uadilifu wakati wa kutoa huduma kwa wananchi.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.
Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo wilayani Ileje yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.
Dkt. Ndumbaro ametoa wito huo kwa watumishi hao wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, ikiwa ni pamoja na kusikiliza na kutatua kero na changamoto zinazowakabili watumishi walio katika wilaya hizo zilizoko pembezoni.

Dkt. Ndumbaro amewaambia watumishi hao kuwa uadilifu unajengeka kwa kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma na kuongeza kuwa, wakizingatia hayo hakutakuwa na upendeleo wakati wa utoaji huduma kwa wananchi na watumishi wanaohitaji huduma za kiutumishi kwa waajiri.

Dkt. Ndumbaro ameongeza kuwa, wakati wa utoaji wa huduma kwa wananchi, watumishi hao wanapaswa kuhakikisha wanazingatia Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2005 ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, Bw. Haji Musa Mnasi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya halmashauri yake kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo wilayani Ileje yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.
Mwalimu Elius Majoba wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje akiwasilisha changamoto yake ya kiutumishi kwa kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo wilayani Ileje yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.

Aidha, Dkt. Ndumbaro ametumia fursa hiyo kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili watumishi wa Wilaya za Ileje na Momba na kuzipatia ufumbuzi ili kuwawezesha watumishi hao kufanya kazi kwa weledi pasipo kuwa na changamoto ambazo kwa namna moja au nyingine zitakwamisha utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kuhusu changamoto ambazo zinahitaji muda, viambatisho au vielelezo muhimu, Dkt. Ndumbaro amezichukua ili zikafanyiwe kazi na ofisi yake mapema iwezekanavyo na kuwaahidi kuwapatia mrejesho watumishi hao huku akiwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii wakati akishughulikia kero na changamoto zao.

Akishiriki kutatua kero za watumishi hao, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Mathew Kirama amemtaka Katibu wa TSC Wilaya ya Ileje kufuatilia jalada la Mwalimu Kostadi Kasunga Makao Makuu ya TSC ili kumuwezesha mtumishi huyo kupata taarifa zake muhimu za kiutumishi alizozipoteza baada ya jarada lake kupotea mahala pa kazi.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Mathew Kirama akijibu hoja za kiutumishi zilizowasilishwa na watumishi wa Wilaya ya Ileje wakati wa ziara ya kikazi ya Dkt. Laurean Ndumbaro yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Dkt. Seif Shekalaghe akimshukuru Dkt. Ndumbaro kwa kufanya ziara ya kikazi wilayani Momba na Mkoa wa Songwe kwa ujumla yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma mkoani humo.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.

Kufuatia maelekezo hayo, Mwalimu Kostadi Kasunga amemshukuru Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro kwa ziara yake ya kikazi ambayo imekuwa ni chachu ya utatuzi wa changamoto za kiutumishi zinazowakabili watumishi walio katika wilaya hiyo.

Naye Bw. Ntuale Mwakabanje ambaye ni Afisa Muuguzi Msaidizi Mkuu wilayani Ileje amemshukuru Dkt. Ndumbaro kwa kufanya ziara katika halmashauri hiyo iliyopo pembezoni kwa lengo la kuzifanyia kazi changamoto na kero zinazowakabili kiutendaji.
Afisa Biashara, Bw. Maximillan Mtui wa Halmashauri ya Wilaya ya Momba akiwasilisha changamoto za kiutumishi kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu huyo wilayani Momba yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Mathew Kirama akijibu hoja za kiutumishi zilizowasilishwa na watumishi wa Wilaya ya Momba wakati wa ziara ya kikazi ya Dkt. Laurean Ndumbaro yenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa wilaya hiyo.

Mara baada ya Katibu Mkuu kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili Watumishi wa Umma wilayani Momba, Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Dkt. Seif Shekalaghe amemshukuru Dkt. Ndumbaro kwa kufika wilaya ya Momba ambayo iko pembezoni na kuongeza kuwa kitendo hicho kinadhihirisha kwamba yeye ni Katibu Mkuu wa UTUMISHI anayewajali watumishi wote bila kujali mazingira waliyopo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Songwe, yenye lengo la kuhimiza utendaji kazi wenye matokeo ambao Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anautaka katika utawala wake, Sanjali na hilo Dkt. Ndumbaro ametatua changamoto na kero zinazowakabili watumishi wa mkoani humo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news