BREAKING News: Mdude Nyangali wa CHADEMA aachiwa huru

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Mahakama ya Hakimu mkazi Mbeya, imemuachia huru mwanaharakati wa demokrasia na mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mdude Nyangali baada ya kutompata na hatia katika kesi ya madawa ya kulevya iliyokuwa ikimkabili. 

Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer amesema leo Juni 28,2021 kuwa, upande wa Jamhuri ulishindwa kutoa ushahidi wa kutosha kumtia Mdude hatiani.
Awali Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya iliahirisha kusoma hukumu ya kesi ya kada huyo iliyokuwa itolewe Juni 14, 2021.

Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer siku hiyo alisema ameiahirisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake na kubainisha kuwa hukumu hiyo itasomwa Juni 28, 2021.

Mdude alikuwa anakabiliwa na shtaka la kusafirisha heroin gramu 23.4 mwaka 2020.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news