Mashindano ya MISS EAST AFRICA kufanyika Novemba, mwaka huu

MASHINDANO ya kumsaka Miss East Africa 2021, yanatarajia kufanyika Novemba, mwaka huu, jijini Dar es Salaam na kushirikisha nchi 15.

Makamu wa Rais wa mashindano hayo Jolly Mutesi alisema ni fursa nzuri kwa Tanzania ina kujitangaza kupitia utalii na uwekezaji na kwamba yameandaliwa Rena Events Limited ya mkoani Dar es Salaam.
Mutesi ambaye yupo nchini kwa ziara wiki mbili kwa ajili ya maandalizi ya awali alisema, mashindano hayo ni makubwa ya urembo kwa ukanda wa Afrika Mashariki yakitarajiwa kuangaliwa na watu wengi duniani. 

Amesema, mashindano hayo yayarishwa mibashara kupitia televisheni, akitoa wito kwa makampuni mbalimbali yanayohitaji kutangaza biashara zao ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kupitia mashindano hayo.  

Mutesi amezitaja nchi washiriki kuwa ni Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Djibouti na Tanzania.  

Nyingine ni Somalia, Madagascar, Malawi, Ushelisheli, Sudan Kusini, Comoro na Mauritius. 

Mashindano hayo yalibuniwa na kuanzishwa na Rena Callist yalianza mwaka 1996 na kuwahi kufanyika Burundi kwa udhamini wa Hayati Rais Piere Nkurunzinza.

“Kuanzia sasa mashindano ya Miss East Africa yatakuwa yakifanyika kila mwaka, yatasaidia katika kudumisha umoja wa Afrika Mashariki, kukuza utalii, kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji,”amesema Mutesi.  

“Mashindano pia yatatoa elimu na kusaidia katika changamoto mbalimbali hasa zinazowakabili wanawake na watoto wa ukanda huu wa Afrika ya Mashariki,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news