DC Mgandilwa:Acheni kuwarubuni watoto wasifanye vizuri katika mitihani

Na Hadija Bagasha, Tanga

Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Hashim Mgandilwa ametoa onyo kali kwa wazazi na walezi wenye tabia za kuwarubuni watoto wao wasifanye vizuri katika mitihani ya kuhitimu elimu yao ya msingi, kwani kufanya hivyo kunapelekea kushindwa kufikia ndoto zao za kupata elimu.
Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Raskazone English Medium, Ally Rashid,akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Tanga, Hashim Mgandilwa zawadi kama sehemu ya kuunga mkono sekta ya elimu nchini. (Picha na Hadija Bagasha).
Mkuu huyo wa wilaya ameyasema hayo wakati alipokuwa katika makao makuu ya Taasisi ya Raskazone English Medium iliyopo jiji Tanga ambapo amesema kuwa ipo changamoto kubwa kwenye elimu kutoka kwa wazazi kwa kuwakatishia watoto ndoto zao.

DC Mgandilwa amesema kuwa, Wilaya ya Tanga na mkoa kwa ujumla kuna changamoto kubwa kwenye masuala ya elimu kwa kuwa wapo wazazi wanaodiriki kuwarubuni watoto wao wafanye vibaya kwenye mitihani yao ili wasiweze kujiendeleza na elimu ya mbele.

Hivyo aliwataka wazazi kubeba wajibu wao wa kuhakikisha watoto wanaporudi nyumbani wanasimamia maendeleo yao na kuwafuatilia kwa ukaribu ili kuwafanya watoto wenyewe waamini kwamba shule ni muhimu katika maisha yao.

“Ndugu zetu wazazi wilaya yetu ya Tanga na Mkoa wetu Tanga tuna changamoto kubwa katika masuala ya elimu wazazi, wanafunzi kumekuwa na mtihani mkubwa sana wanafunzi wanaanza shule lakini kumaliza inakuwa mtihani wapo wazazi wanaodiliki kuwaambia watoto wafanye vibaya wanapokuwa wanafanya mitihani yao ili watoto wasiendelee na elimu yao ya mbele,”amesema Mgandilwa.
Hata hivyo DC Mgandilwa ameipongeza Taasisi hiyo ya Raskazone English medium kwa kuweza kuwafundisha wanafunzi hao kubobea katika masomo ya sayansi kwani wameonyesha uwezo mkubwa na kuwashauri kuendelea kuwa nao bega kwa bega kwani dunia ya sasa inahitaji wasomi wa masomo ya sayansi hivyo amefurahishwa na ubunifu mkubwa uliofanywa na wanafunzi shuelni hapo.

“Serikali haina uwezo wa kufanya kila kitu inahitaji msaada wa Private sekta kwajili ya kuondoa baadhi ya changamto ambazo zipo kwenye maeneo yetu kwahiyo kitendo cha kuwekeza katika sekta hii hapa Tanga mimi niwatie moyo na niwaahidi kuwa serikali ya Mkoa wa Tanga itawapa ushirikiano kila mtakapohitaji,”alisema DC Mgandilwa.

"Niwapongeze kwa uamuzi mzuri Kitendo cha kuamua kuufanya wa kuwekeza Taasisi hii hapa Tanga lakini pia kuwekeza kwenye elimu tunajua taasisi zetu hizi za shule ni huduma lakini pia mnaziendesha ili kupata chochote leo hii nimeshuhudia huduma nzuri mnayoitoa kwa watoto wetu niwatie moyo muendelee hivyo hivyo,”alisema DC Mgandilwa.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo, Ally Rashid amesema shule hiyo ilianzishwa ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kutoa elimu bora kwa raia wake ili waweze kumudu ushindani katika soko la ajira kimataifa.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa shule hiyo imeweka walimu wa kutosha wenye weledi wa kufundishwa masomo yote kama unavyoelekeza mtaala wa elimu ya msingi Tanzania, lakini pia shule hiyo imefanikiwa kutekeleza malengo yake kwa asilimia 99 ikiwemo kusaidia pamoja na serikali katika kutoa elimu bora miongoni mwa malengo mengine.

“Tumefanikiwa kuwa na ufaulu mzuri na unaoridhisha katika mitihani ya ndani ya kujipima na ya nje kama mock na mitihani ya taifa Necta ya darasa la nne na la saba katika awamu zilizopita ambapo kwa awamu hii wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba 2021, ni 68, wamefanikiwa kumaliza elimu ya msingi,”amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news