Naibu Meya wa Manispaa ya Musoma Haji Mtete, kamati wakagua miradi ya maendeleo

Na Fresha Kinasa, Diramakini Blog

Diwani wa Kata ya Nyasho ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Musoma, Haji Mtete pamoja na Kamati ya Siasa ya Kata ya Nyasho wamefanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika kata hiyo iliyotekelezwa kuanzia mwezi Januari hadi Juni na kubaini miradi hiyo kutekelezwa kwa ufanisi.
Diwani wa Kata ya Nyasho, Haji Mtete mwenye mtandio shingoni akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya kata ya Nyasho kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyasho wakiwa katika chumba cha maabara wakikagua.
Ziara hiyo imefanyika Septemba 9, 2021 ambapo Wajumbe wa kamati hiyo walifika katika Shule ya Sekondari Nyasho na kupokea taarifa ya ujenzi vyumba viwili vya maabara ya Biolojia na Kemia ambavyo vipo katika hatua ya mwisho kuanza kutumiwa na wanafunzi wa shule hiyo kufuatia Serikali kuu kutoa shilingi milioni 30 kumalizia ujenzi wa vyumba hivyo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyasho, Matiko Seruka ameieleza kamati hiyo kuwa, walipokea fedha Shilingi Milioni 30 kutoka Serikali Kuu ambazo zimefanya kazi mbalimbali za ukamilishaji wa vyumba viwili. Na kwa sasa kilichobakia ni uwekaji wa umeme na maji katika vyumba hivyo na baada ya hatua hiyo, wataomba vifaa serikalini ili wanafunzi waanze kutumia maabara hizo.

"Tuzilipata fedha kutoka Serikali Kuu kutokana na maboma kuwa tayari baada ya Wananchi kuchangia, tupo kwenye hatua ya kuomba vifaa ili shughuli ya utumiaji wa maabara hizi uanze kufanyika. Hii ni hatua kubwa sana ujenzi wa maabara hizi kufikia kiwango kizuri cha ukamilifu,"amesema Matiko.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyasho katikati akitoa ufafanuzi kwa Viongozi wa Kamati ya Siasa Kata ya Nyasho walipotembelea kukagua ujenzi wa vyumba vya maabara shuleni hapo. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nyasho, Fidelis Manyerere na kushoto kwake Haji Mtete Diwani wa Kata ya Nyasho.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyasho katikati akitoa ufafanuzi kwa Viongozi wa Kamati ya siasa kata ya Nyasho walipotembelea kukagua ujenzi wa vyumba vya maabara shuleni hapo. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nyasho, Fidelis Manyerere na kushoto kwake Haji Mtete Diwani wa kata ya Nyasho.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyasho katikati akitoa ufafanuzi kwa Viongozi wa Kamati ya Siasa Kata ya Nyasho walipotembelea kukagua ujenzi wa vyumba vya maabara shuleni hapo. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nyasho Fidelis Manyerere na kushoto kwake Haji Mtete Diwani wa Kata ya Nyasho.
Diwani wa Kata ya Nyasho, Haji Mtete amepongeza juhudi za Wananchi wa kata hiyo waliochangia ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyumba hivyo vya maabara na kuiwezesha Serikali kuleta fedha ambazo zimewezesha ukamilishaji wake. Huku akiwaomba pia kuendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo pasipo kusukumwa na serikali.

Pia, Mtete amewahakikishia Wananchi wa Kata ya Nyasho kuwa, ataendelea kuwapa ushirikiano wa dhati na kuwatumikia kuwaletea maendeleo na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa ufanisi unaotakiwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Kata ya Nyasho, Fidelisi Manyerere akizungumza na Walimu wa Shule ya Sekondari Nyasho, amewataka walimu wa shule hiyo kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika kuhakikisha kwamba, wanafunzi wanafanya vizuri katika masomo yao.
Viongozi wa Kamati ya Siasa Kata ya Nyasho wakikagua jengo la maabara ya Fizikia ambalo bado halijakamilika. Huku maabara ya Biolojia na Kemia zikiwa tayari katika hatua ya mwisho kuanza kutumika.
Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Siasa kata ya Nyasho kulia ni Diwani wa Kataata ya Nyasho Haji Mtete mwenye mtandio shingoni.
Diwani wa kata ya Nyasho Haji Mtete kulia na kushoto ni Wajumbe wa Kamati ya siasa ya kata ya Nyasho wakiwa katika daraja la Nyakisaka walipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya Maendeleo ndani ya kata hiyo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Nyasho Fidelis Manyerere akizungumza na Walimu wa Shule ya Sekondari Nyasho (hawapo pichan).
Diwani wa kata ya Nyasho Haji Mtete akizungumza na Wanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Nyasho alipofika shuleni hapo akiwa ameambatana na Kamati ya siasa ya kata hiyo kukagua ujenzi wa vyumba vya maabara.
Pia, Manyerere amemtaka Mkuu wa Shule hiyo kupanga mipango kwa kushirikiana na Wazazi kusudi kuchangia maendeleo ya shule hiyo kwa hiari ili kuchochea ufaulu kwa kiwango bora.

Aidha, kamati hiyo pia imefanya ukaguzi wa madaraja mawili ya Nyakisaka yaliyopo ndani ya Kata ya Nyasho ambayo ni muhimu kwa shughuli za maendeleo ndani ya kata hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news