UJUMBE WA TANZANIA NCHINI CAPE VERDE KATIKA KUTANO WA KIMATAIFA WA UTALII (picha)


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro akimuonesha baadhi ya vivutio vya utalii vilivyopo katika jarida la Utalii kutoka Tanzania Waziri wa Utalii wa Hispania, Maria Illerakabla baada ya kumkabidhi zawadi ya majarida yanayoelezea utajiri wa vivutio vya utalii vilivyopo nchini mara baada kufanya kikao cha ana kwa ana kando ya mkutano wa 64 Kimataifa wa Utalii wa Kanda ya Afrika unaoendelea kufanyika kwa muda wa siku nne katika Kisiwa cha SAL nchini Cape Verde.(Picha zote na WMU).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro akimkabidhi zawadi ya Kitabu cha misitu kinachoelezea fursa za uwekezaji katika maeneo ya misitu nchini Mhe. Ngobitizitha Ndlovu (kushoto) mara baada kufanya kikao cha ana kwa ana kando ya mkutano huo wa Kimataifa wa Utalii wa Kanda ya Afrika unaoendelea kufanyika kwa muda wa siku nne katika Kisiwa cha SAL nchini Cape Verde.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro ( katikati ) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Utalii na Mambo Kale Zanzibar, Mhe.Lela Mussa Mohamed (kushoto) pamoja na Waziri wa Utalii wa Morroco, Mhe.Nadia Fettah ( kulia) mara baada kufanya kikao cha ana kwa ana kando ya mkutano huo wa Kimataifa wa Utalii wa Kanda ya Afrika unaoendelea kufanyika kwa muda wa siku nne katika Kisiwa cha SAL nchini Cape Verde. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiagana na Waziri wa Utalii Cape Verde, Mhe. Carlos Santos ambapo wamekubaliana katika kubadilishana uzoefu katika kukuza utalii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news