Waziri Mhagama afunguka katika harambee shule maalum ya Libermann Viziwi

NA MWANDISHI MAALUM

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameongoza harambee maalumu ya ununuzi wa vifaa maalumu vya kielimu na saidizi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa shule ya Libermann Viziwi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akishiriki maombi maalum ya kuombea Shule ya Libermann Viziwi pamoja na sala maalum ya sikukuu somo wa shule hiyo (Francis Maria Libermann) iliyoambatana na harambee hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Libermann Viziwi mara baada ya kumkabidhi zawadi wakati wa hafla hiyo.
Hafla hiyo ilifanyika tarehe 25 Septemba, 2021 na iliambatana na kumbukumbu ya Somo wa Shule zetu Mwenyeheri Francis Maria Paul Libermann na pamoja na maadhimisho ya wiki ya Viziwi Duniani.

Waziri alionesha kufurahishwa na hatua ya uongozi wa shule hiyo kwa kuona umuhimu wa kusaidia watoto wenye mahitaji maalum na kuendesha harambee hiyo ili kuwa na vifaa na kuboresha masuala yanayowahusu ili kuwa na mazingira rafiki ya ufundishaji na kuhakikisha wanatimiza ndoto zao.

“Nimefurahishwa sana na uamuzi wenu wa kuadhimisha wiki hii ya Viziwi Duniani kwa kufanya harambee ya kupata fedha za uendeshaji na ununuzi wa vifaa maalumu vya kielimu na saidizi kwa wanafunzi wetu Wenye Ulemavu. Hongereni sana,”amesema Waziri Mhagama.

Waziri alieleza kuwa kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, kwa mwaka 2019/2020, Tanzania inakadiriwa kuwa na idadi ya watu milioni 55.9 ambapo milioni 2.5 kati yao ni Watu wenye Ulemavu. Aidha, kwa kipindi kirefu Watu Wenye Ulemavu wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali katika kutafuta fursa na huduma za kijamii ikiwemo elimu.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Libermann Viziwi wakionesha ndoto zao baada ya masomo kwamgeni rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa hafla ya Harambee maalumu ya ununuzi wa vifaa vya shule na saidizi kwa wanafunzi hao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiangalia miundombinu ya kufundishia watoto wenye mahitaji maalum wa shule ya Libermann Viziwi alipotembelea kukagua mazingira ya shule hiyo.anayetoa maelezo ni Bi. Neema Shiyo Mnzava, Mwenyekiti wa Kamati ya Shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akikabidhi mchango wake kwa Bw. Karoli Tarimo, Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee ya ununuzi wa vifaa vya kielimu na saidizi kwa wanafunzi wenye uziwi katika shule ya Libermann Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa na watendaji wa Shule ya Viziwi ya Libermann wakionesha Hundi iliyochangiwa na uongozi wa shule hiyo wakati wa Harambee maalum ya kuchangia vifaa vya shule na vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye uziwi wa shule hiyo, Hafla hiyo ilifanyika tarehe 25 Septemba, 2021 katika shule hiyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akihutubia wakati wa Kilele cha Harambee Maalum ya ununuzi wa vifaa vya kielimu na saidizi pamoja na maadhimisho ya Somo wa Shule za Libermann iliyofanyika Septemba 25, 2021 shule ya Libermann Viziwi iliyopo kata ya Kawe, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.Shule inamilikiwa na Shirika la Mapadri wa Roho Mtakatifu (Spiritans) Kanda ya Tanzania.

“Watu wenye ulemavu wamekuwa wakiachwa nyuma katika masuala mbalimbali likiwemo hili la elimu, niendelee kuiasa jamii kuwapa kipaumbele na kuwawezesha ili wapate elimu itakayotoa fursa ya kuonesha uwezo walio nao bila kujali hali zao,”alisisitiza Waziri Mhagama.

Akisoma taarifa ya shule hiyo Mwalimu Mkuu Bi.Edister Massawe alisema shule inalenga kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuto elimu bora kwa watoto wa Tanzania hasa wenye mahitaji maalum kama vile viziwi pamoja na kuwapa fursa watoto wenye ulemavu kupata elimu bora, kusaidia familia zao kwa kuwapatia ufadhili na udhamini kwa watoto hao ili wajikwamue kielimu.

“Shule hii ya Viziwi inatoa elimu hiyo bure na imejikita kuwasaidia ili kuwafanya wabadilike wawe wenye kujitambua, kugundua na kuendeleza vipaji vyao na kuwajengea uwezo kwenye nyanja za ufundi na biashara ili waweze kushiriki katika masuala ya ujasiriamali, utunzaji wa mazingira na afya,”alisema Edister.
Padre Philip Athanas Massawe C.S.Sp, Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu (Spiritans) Kanda ya Tanzania, akieleza historia ya Shirika wakati wa Harambee maalum ya kuchangia vifaa vya shule na Vifaa saidizi kwa wanafunzi wenye uziwi wa shule hiyo.

Akiongoza ibada maalumu ya kuombea shule na kumbukumbu ya Somo wa Shule zetu Mwenyeheri Francis Maria Paul Libermann Padre Philip Athanas Massawe C.S.Sp, Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu (Spiritans) Kanda ya Tanzania, alisema jamii iwe mstari wa mbele bila uoga kuwainua watu wenye mahitaji maalum kwa kuwajengea ujasiri na kuwatambua kwani kufanya hivyo ni sehemu ya ibada na kujipatia baraka mbele za Mungu kwa kuwaangalia wahitaji.

“Taifa tuondoe uwoga na kuwainua watu wenye ulemavu na kuwaona wanaweza na kuwainua bila kuacha kuwaombea kuyafikia malengo yao,”alieleza Padri Philip
Meneja wa Kampuni ya Jatu PLC Bw. Mohamed Simbano akikabidhi msaada wa mchele kwa uongozi wa Shule ya Libermann Viziwi na katikati ni mgeni rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama.
Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) akitoa burudani ya kuhamasisha uchagiaji wa vifaa vya shule na saidizi kwa wanafunzi wa shule ya Libermann Viziwi.

AWALI

Shule ya Libermann Viziwi inamilikiwa na Shirika la Mapadri wa Roho mtakatifu (spiritans) Kanda ya Tanzania. Shule ipo kata ya Kawe, Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.Shule ilisajiliwa rasmi tarehe 11 Septemba, 2019 na kupewa namba za usajili EM. 17973 yenye kaulimbiu isemayo “Moyo mmoja roho moja (One heart one Soul).Ni shule pekee ya viziwi inayotumia mtaala wa Kingereza kwa kufundishia na kujifunzia na ina uwezo wa kuchukua wanafunzia 210 kuanzia ngazi ya awali mpaka darasa la saba.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news