HIFADHI YA SERENGETI KUENDELEA KUCHANGIA MIRADI YA MAENDELEO-MHE.MARY MASANJA

Na Happiness Shayo-WMU

Hifadhi ya Taifa ya Serengeti itaendelea kuchangia miradi ya maendeleo katika vijiji saba vinavyoizunguka hifadhi hiyo ili kuinua uchumi wa wananchi wanaoshi katika maeneo hayo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe. Mary Masanja (Mb) alipokuwa akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo kwenye ziara ya Mawaziri 8 wa Kisekta leo.

Amesema kuwa kutokana na wananchi wa vijiji hivyo kutunza vizuri hifadhi hiyo, Serikali itaendelea kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Mwaka huu wa fedha tumetenga fedha za ujenzi wa madarasa mawili katika kijiji cha Kisangula, nyumba mbili za waganga na bwawa la kunyweshea mifugo katika kijiji cha Nyansulula na ukarabati wa bwawa katika eneo la Machocho.

Pia, Mhe. Masanja ameongeza kuwa Serikali itajenga kituo cha afya , nyumba za waganga na madarasa mawili katika kijiji cha Mbalibali, nyumba za waganga mbili, katika kijiji cha Tamkeni na madarasa mawili katika kijiji cha Nyambuli.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news