Sarah Magesa: Watanzania tuzidi kumngoja Mungu katika nyakati zote za maisha yetu

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Watanzania wameombwa kuwa na tabia ya kumngoja Mungu katika vipindi mbalimbali ambavyo wanakutana navyo kila wakati katika maisha yao.

Hayo yamesemwa na Mwimbaji wa Nyimbo za Injili kutoka Tanzania, Sarah Magesa kupitia wimbo wake mpya uitwao Bado Nakungoja.

Sarah amesema, kuna wakati Watanzania tunapitia vipindi vigumu na vingine vyepesi, kikubwa ni kuendelea kumngoja Mungu kwa Saburi.

"Ukiangalia kama nchi tunapitia vipindi tofauti vingine vinavunja Moyo na vingine vinaumiza kama wakati huu wa Ugonjwa wa Corona, tusiache kumtegemea na kumngoja Mungu atushindie,"amesema Sarah Magesa.
Wimbo wake Sarah Magesa uiitwao Bado Nakungoja umerekodiwa hivi karibu na ukiwa na ujumbe wa kuwasihi watu wote kuwa na tabia ya kumngoja Mungu katika mambo yote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news