WATENDAJI WA TAASISI ZA UMMA KANDA YA ZIWA WATAKIWA KUWASILISHA NYARAKA ZINAZOTAKIWA KUTUNZWA KATIKA KITUO CHA KUMBUKUMBU KANDA YA ZIWA MWANZA

Na James K. Mwanamyoto - Mwanza

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma zilizoko Kanda ya Ziwa kuhakikisha wanawasilisha nyaraka zenye umuhimu kitaifa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Na. 3 ya Mwaka 2002.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na Watumishi na wageni waalikwa kabla ya kuzindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa jijini Mwanza.

Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo wakati akizindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa kilichopo jijini Mwanza.

Mhe. Mchengerwa amesema waajiri wanao wajibu wa kuhamishia kumbukumbu zote muhimu katika kituo hicho ili ziweze kutunzwa kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa kwa ajili ya matumizi ya sasa na vizazi vijavyo.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, miundombinu ya kituo hicho cha Kumbumbuku alichokizindua ni ya kisasa inayowezesha kutunza kumbukumbu za nyaraka kidijitali.
Sehemu ya Watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuzindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa jijini Mwanza.

“Kituo hiki kina uwezo mkubwa wa kuhifadhi majalada, hivyo kitawezesha taasisi zote za umma kuokoa zaidi ya mita za mraba 16,600 za ofisi zao ambazo zingetumika kuhifadhi majalada hayo,” Mhe. Mchengerwa amefafanua.

Akizungumzia lengo la uanzishwaji wa kituo hicho kwa niaba ya Katibu Mkuu-UTUMISHI, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Francis Michael amesema ujenzi wa kituo hicho ni mwendelezo wa juhudi za Serikali za kuhakikisha kuwa taarifa, kumbukumbu na nyaraka zinazalishwa katika mifumo iliyokubalika kwa mujibu wa sheria na miongozo iliyopo ikiwa ni pamoja na kutuzwa katika mazingira bora na salama kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi amesema Kituo hicho cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa kitaunganishwa na mifumo ya Serikali Mtandao, hivyo nyaraka zinazokusanywa na kuhifadhiwa zitawekwa katika mifumo ya kidijitali.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Francis Michael akielezea lengo la Serikali la kujenga Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa kilichopo jijini Mwanza.

Bw. Msiangi ameongeza kuwa, nyaraka zinazozalishwa na taasisi za umma katika mifumo ya kidijitali zitapokelewa moja kwa moja kidijitali kutoka katika taasisi za umma.

Naye, Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa aliyetafuta kiwanja mwaka 1982 ambacho Kituo hicho kimejengwa, Mzee Silvin Mongella ameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kutoa fedha za kujenga kituo cha kuhifadhi kumbukumbu Kanda ya Ziwa.

Mzee Mongella amewahimiza watumishi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kufanya kazi kwa bidii kwani hivisasa nyaraka ni nyingi na zinahitaji kuhifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo na kuongeza kuwa, wasipotekeleza wajibu wao kikamilifu watawanyima haki Watanzania kujua utamaduni wao na historia yao.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi, akitoa maelezo ya awali kuhusu Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa kilichopo jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa ambaye pia ni mwasisi wa Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa, Mzee Silvin Mongella akielezea historia ya upatikanaji wa kiwanja ambacho Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa kimejengwa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akikata utepe kuzindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa jijini Mwanza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akisoma ujumbe wa kibao cha uzinduzi wa Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa mara baada ya kuzindua kituo hicho jijini Mwanza. Pembeni yake ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiangalia mchoro wa Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa baada ya kuzindua kituo hicho jijini Mwanza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiangalia moja ya nyaraka zilizoko katika Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa baada ya kuzindua kituo hicho jijini Mwanza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa baada ya Mhe. Mchengerwa kuzindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa jijini Mwanza.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezindua Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Ziwa Mwanza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kituo ambacho kinatoa huduma katika Mikoa sita ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Kagera.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news