Waziri Ummy Mwalimu asitisha kwa muda matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji ada za Maegesho ya Magari

NA GODFREY NNKO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ummy Mwalimu amesitisha kwa muda ukusanyaji wa ada za maegesho ya magari kwa kutumia mfumo mpya wa kieleketroniki.

Mfumo huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).
WAZIRI WA OR- TAMISEMI, UMMY MWALIMU

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais (OR-TAMISEMI), Nteghenjwa Hosseah imeeleza kuwa Waziri Ummy amesitisha mfumo huo kuanzia leo Jumamosi Oktoba 9, 2021 na kuagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Professa Riziki Shemdoe kukutana na timu ya wataalamu TARURA kujadili namna ya kutatua changamoto zilizojitokeza.

“Wakati hayo yakiendelea ukusanyaji wa ada za maegesho ya magari zitaendelea kukusanywa kwa kutumia mfumo wa awali (manual system) ambao ulikua unatumika kukusanyia ada hiyo kabla ya kuanza kutumia mfumo wa kielektroniki (TeRMIS),” imeeleza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news