Chriss Mugalu wa Simba SC arejea nyumbani

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Chriss Mugalu ambaye ni mshambuliaji wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC amerudi nchini kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Mshambuliaji huo amerudi nyumbani kwa ajili ya kujiuguza huku akisema atarudi akiwa imara zaidi hapo baadae, Mungu akimjalia afya njema.

Mugalu alipata majeraha wakati Simba SC ikiwa kwenye maandalizi ya kucheza dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana mwezi uliopita ambapo hajarejea uwanjani tangu wakati huo.

Amesema, amelazimika kurudi nyumbani kwao ili apate muda wa kupumzika na kuendelea na tiba zaidi.

“Bado sijafahamu naweza kurejea wakati gani uwanjani , lakini matibabu ambayo nayafanya sasa ni ya hali ya juu na natakiwa kupumzika muda mwingi ndio maana nimerudi nyumbani,"amesema.

Mshambuliaji huyo alimaliza nafasi ya pili katika orodha ya wafungaji bora msimu uliopita 2020/21, akitanguliwa na mshambuliaji mwenzake wa Simba SC John Bocco.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news