Viongozi wa REA Tanzania watembelea Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa Kutumia Maporomoko ya maji ya Mto Ruaha mkoani Njombe



Msimamizi wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme wa maji ya Mto Ijangala, Mhandisi Lydia Malaki (aliyevaa ‘reflector’) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (mwenye fulana ya bluu), hatua mbalimbali za ujenzi wa mradi huo wakati wa ziara ya Menejimenti ya REA iliyofanyika Novemba Mosi, 2021 katika Wilaya ya Makete mkoani Njombe. Mradi huo unasimamiwa na KKKT kupitia kampuni ya Nishati Lutheran Associate na imepatiwa ruzuku ya takribani shilingi milioni 400 kutoka REA.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (wa pili –kushoto) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Matembwe Village inayosimamia Mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Ruaha uliopo katika Kijiji cha Ikondo, Mkoa wa Njombe, Johhanes Kamonga (wa tatu – kushoto), wakati wa ziara ya viongozi wa REA kutembelea vyanzo vya kuzalisha nishati ya umeme katika mradi huo, Oktoba 31, 2021. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi, Mhandisi Jones Olotu wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji wa Masoko na Teknolojia, Mhandisi Advera Mwijage. Kampuni ya Matembwe Village imepata ruzuku ya shilingi milioni 700 kutoka REA ambapo jumla ya wateja 586 wameunganishiwa umeme.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (wa tano kutoka kulia waliosimama) na Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Kusini Kati, Mhashamu Wilson Sanga (wa nne kutoka kulia - waliosimama), wakiwa katika picha ya pamoja na wananchi na viongozi wa Kijiji cha Masisiwe wakati wa ziara ya Menejimenti ya REA kutembelea Mradi wa kuzalisha umeme wa maji ya Mto Ijangala uliopo katika kijiji hicho, Wilaya ya Makete mkoani Njombe, Novemba Mosi, 2021. KKKT kupitia kampuni ya Nishati Lutheran Associate imepata ruzuku ya takribani shilingi milioni 400 kutoka REA kwa ajili ya Mradi huo ambao upo katika hatua ya ujenzi. (Picha zote na REA).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news