Watakiwa kusimamia matumizi ya fedha za Serikali katika halmashauri

NA ANGELA MSIMBIRA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe.Ummy Mwalimu ameziagiza Sekretarieti za Mikoa zote nchini kuhakikisha wanasimamia, wanazishauri na kutoa maelekezo kwa halmashauri katika kutekeleza miradi ya maendeleo
Akiongea na Sekretarieti ya Mkoa wa Iringa, Waziri Ummy amesema Sekretarieti za Mkoa zina wajibu wa kuzisimamia halmashauri na kuhakikisha halmashauri zinatekeleza majukumu yao ya kuleta maendeleo kwa wananchi.

Waziri Ummy amesema, Sekretarieti za Mikoa nchini ndio kiungo muhimu katika kuhakikisha miradi ya halmashauri inatekelezwa kwa wakati na inalengo ya kutatua kero za wananchi

Amewaelekeza wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa na kupokea maelekezo na kuyatekeleza kwa wakati ili kuleta maendeleo katika Mikoa yote nchini

"Ninawategemea sana Sekretarieti za Mikoa katika kuhakikisha wa akagua miradi ya maendeleo nayotekelezwa na halmashauri kwa kuwa nyinyi ndio kiungo. Muhimu katika utekelezaji wa miradi,"amesema Waziri Ummy.

Amewataka kuhakikisha wanasimamia matumizi ya fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri kwa kukagua na kusimamia utekelezaji miradi hiyo.

Amezitaka Sekretarieti za Mikoa kusimamia ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha za serikalli ili ziweze kutumika katika kutatua kero za wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news