Naibu Waziri Ndejembi amchangia fedha ya nauli na ya kununulia vifaa vya shule mlengwa wa TASAF

NA VERONICA MWAFISI

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amemchangia fedha ya nauli na ya kununulia vifaa vya shule mlengwa wa TASAF Bi. Siwema Chikawe, ambaye amewezeshwa na mpango wa TASAF kupata elimu ya Msingi, kidato cha kwanza mpaka cha nne na kwa sasa yupo kidato cha tano katika Shule ya Sekondari mojawapo iliyopo Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na wananchi na walengwa TASAF wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.
Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Mhe. Ndejembi ametoa mchango huo, wakati akizungumza na wananchi na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika Kijiji cha Kiparang’anda Wilayani Mkuranga.

Mhe. Ndejembi amesema, ameshawishika kumchangia mwanafunzi huyo kutokana na kazi nzuri iliyofanya na mratibu wa TASAF wilayani hapo na TASAF Makao Makuu kwa kumpatia ruzuku iliyomuwezesha kuendelea na masomo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akijibu hoja za walengwa wa TASAF wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Akihimiza umuhimu wa elimu kwa walengwa wa TASAF, Mhe. Ndejembi amemtaka mlengwa huyo kutekeleza wajibu wake kwa kuhakikisha anasoma kwa bidii ili hapo baadae aweze kuwa msaada wa kuikwamua familia yake kutoka katika lindi la umaskini.

“Hakikisha unazingatia masomo ili upate ufaulu mzuri utakaokuwezesha kujiunga na elimu ya juu kwa manufaa yako binafsi, familia yako na Taifa kwa ujumla”, Mhe. Ndejembi amesisitiza.
Mlengwa wa TASAF Bi. Siwema Chikawe akitoa ushuhuda kwa Naibu Waziri Mhe. Deogratius Ndejembi wa namna TASAF inavyomuwezesha kupata mahitaji ya Shule, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Kwa upande wake mlengwa huyo wa TASAF Bi. Siwema Chikawe, ameishukuru TASAF kwa kumuwezesha kupata mahitaji ya Shule kwani wazazi wake hawana uwezo wa kumsomesha.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akipokea zawadi ya bidhaa zinazotengenezwa na walengwa wa TASAF Wilayani Mkuranga wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF Wilayani humo.

Akieleza sababu ya familia yake kutokuwa na uwezo wa kumsomesha, Bi. Chikawe amesema baba yake mzazi hana uwezo wa kuona wakati mama yake mzazi hana kazi rasmi ya kumuingizia kipato cha kumuwezesha kumudu gharana za masomo yake.

Mhe. Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Mkuranga yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Mpango wa TASAF unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news