Simba Queens watembeza dozi Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

MABINGWA watetezi, Simba Queens wameendelea kugawa dozi kwa wapinzani katika Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara baada ya kuichapa Oyster-bay Girls 8-0 jioni ya leo Uwanja wa Mo Simba Arena uliopo Bunju jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Simba Queens yamefungwa na Aisha Djafar matatu, Opa Clement na Aisha Mnunka kila mmoja mawili, wakati la nane Oysterbay Girls walijifunga. 

Kwa upande wa watani wao, Yanga Princess wamelazimishwa sare ya 1-1 na wenyeji, Fountain Gate Princess Uwanja wa Fountain Gate, Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news