Clatous Chama arejea Simba SC

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

KLABU ya Simba imetangaza kurejea tena kikosini kwa Kiungo mshambuliaji kutoka Zambia, Clatous Chama akitokea RS Berkane ya Morocco alikokwenda huko miezi mitano iliyopita.
Chama alijiunga na Simba mwaka 2018 na kuondoka mwaka 2021 kabla ya kurejea Simba na kutambulishwa rasmi leo.

Kupitia bango kubwa lililotolewa na Simba likiwa na picha ya Chama limesomeka kwa,“Karibu nyumbani, Welcome home” .

Mshambuliaji huyo aliondoka Simba SC Agosti 13, 2021 na kujiunga na Klabu ya RS Berkane ya Morocco na sasa anarejea baada ya kudaiwa kushindwa kuzoea mazingira nchini Morocco.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news