Makamu wa Kwanza wa Rais atoa wito kwa vyuo vikuu vya Zanzibar

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, amesema jukumu kubwa la vyuo vikuu ni kusaidia kutatua matatizo ya jamii, kwa kufanya tafiti ili kutoa mwangaza na muelekeo wa maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Othman ametoa wito kwa vyuo vikuu vya Zanzibar kufuatilia kwa karibu maeneo mengine ya kupewa kipaumbele cha utafiti kama yalivyoainishwa katika Agenda ya Utafiti ya Zanzibar (Zanzibar Research Agenda).Soma kwa kina hapa>>>

“Hapa tunajifunza dhima na jukumu la kila chuo kikuu kuzingatia umuhimu wa kufanya tafiti zenye tija, ili kuyakabili matatizo sugu yanayokabili jamii na hasa nchi zetu ndani ya Bara la Afrika,”amesema Mheshimiwa Othman.

Mheshimiwa Othman ameshauri kwamba kutokana na ongezeko la vyuo vikuu nchini hali ambayo inapelekea kuongeza ushindani wa udahili na kuwania wanafunzi, ni vyema kujipanga kwa kuweka mikakati imara na juhudi endelevu ili kukitangaza chuo, ikiwemo utoaji wa ‘courses’ zinazovutia, zenye soko duniani sambamba na wahitimu bora wanaoajirika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news