Salamu MAALUM za pongezi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwenda kwa Katibu Mkuu mteule Wizara ya Nishati


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni taasisi ya Serikali iliyopo chini ya Wizara ya Nishati ambayo inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika upatikanaji wa nishati ya umeme vijijini.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Said wakati akikabidhiwa ofisi na Mtangulizi wake, Mhandisi Amos Maganga, Oktoba 29, 2021 aliwaasa watumishi kufanya kazi kwa bidii, maarifa na uadilifu.

Mhandisi Said alisema, matumaini ya Watanzania, hasa wa vijijini, yanategemea dhamana ambayo REA imepewa.

“Tukitetereka katika kutimiza majukumu yetu, tutafifisha matumaini ya Watanzania wengi ambao wanategemea nishati kama nyenzo ya kubadilisha maisha yao,” alisisitiza Mhandisi Said.

Maono ya Mkurugenzi Mkuu REA,ni mwelekeo chanya kupitia Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambayo imedhamiria kuwaletea maendeleo wananchi kuanzia vijijini hadi mijini.

Mheshimiwa Rais Samia anaamini kila mtumishi na Watanzania wakitimiza wajibu na majukumu yao kwa ufanisi,Taifa litapata maendeleo ya haraka ikiwa ndiyo dhamira ya Serikali anayoiongoza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news