TANESCO YATOA TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA UMEME KATIKA BAADHI YA MAENEO NCHINI

NA MWANDISHI MAALUM

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linawafahamisha wateja wake wa mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Tabora, Simiyu na Geita, kuwa leo Jumatano Januari 12, 2022, saa 3:00 asubuhi kumetokea kukosekana kwa huduma ya umeme.
SABABU: Hitilafu kwenye kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Zuzu Dodoma.

JITIHADA: Wataalam wetu wanaendelea na jitihada za kurejesha umeme na tutaendelea kutoa taarifa zaidi. 

Tunawaomba radhi wateja wetu kwa usumbufu utakaojitokeza. 

Mitandao ya kijamii:

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetutz, 

Facebook https://www.facebook.com/tanescoyetutz 

IMETOLEWA NA;

Ofisi ya Uhusiano,

TANESCO MAKAO MAKUU.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news