Karatu kutumia Bilioni 41.8/- mwaka wa fedha 2022/2023

NA SOPHIA FUNDI

HALMASHAURI ya Wilaya ya Karatu mkoani Arusha imepanga kutumia kiasi cha shilingi bilioni 41.8 katika mwaka wa fedha 2022/2023.Akisoma bajeti hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi, Afisa Mipango wa halmashauri hiyo, Rosemary Samson alifafanua kuwa kati ya kiasi hicho mishahara ni shilingi bilioni 26,095,290,000, matumizi ya kawaida sh.bilioni 2,685,519,200,miradi ya maendeleo sh.bilioni 11,927,766,800 huku mapato lindwa yakiwa sh.bilioni 1,166,424,800.

Alisema kuwa, bajeti hiyo imeongezeka kwa asilimia 8.2 ukilinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 ya sh.bilioni 38,264,061,000 kutokana na nyongeza ya mishahara na mapato ya ndani.

Aidha, alisema kuwa Halmashauri ya Wilaya inakadiria kukusanya sh.bilioni 4.5 kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Alitaja vipaumbele vya bajeti kuwa ni kumalizia miradi viporo hasa iliyotumia fedha za Serikali,kuongeza miundombinu mbalimbali katika sekta za elimu msingi na sekondari,afya na kubuni vyanzo vipya vya mapato ya ndani.

Akizungumza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Karia Magaro aliwaomba madiwani kushirikiana na wataalamu kusimamia miradi iliyotengewa bajeti katika kata zao kwani alisema jukumu la kusimamia miradi ya maendeleo katika kata ni la viongozi wa kata na vijiji wakiwemo madiwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news