MHESHIMIWA MARY MASANJA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUMEGA MAENEO YA HIFADHI

NA HAPPINESS SHAYO-WMU

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amewataka wananchi kuacha kuomba kumegewa maeneo ya Hifadhi ili kuepukana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu.
Amesema hayo leo katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alipompa nafasi ya kujibu kuhusu changamoto ya wanyama wakali na waharibifu mkoani humo.

Amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo, vikosi kazi vitatumwa katika maeneo yenye changamoto ya wanyama wakali na waharibifu.

Aidha,ameahidi kutekeleza maelekezo ya Rais ya kuhakikisha Wizara inaweka Kambi ya kudumu kwenye maeneo yenye changamoto ya wanyama wakali na waharibifu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news