Rais Samia kufanya ziara ya kikazi nchini Ufaransa, Ubelgiji

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anatarajia kuondoka nchini kuelekea Ufaransa na baadae Ubelgiji kwa ajili ya ziara ya kikazi katika nchi hizo.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 9,2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus.
Amesema kuwa, Rais Samia akiwa nchini Ufaransa anatarajiwa kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaojadili kuhusu Rasilimali Bahari Duniani.

Pia Rais Samia atashuhudia utiaji saini baina ya Serikali ya Tanzania na Ufaransa katika sekta za miradi ya maendeleo, ushirikiano katika masuala ya uchumi wa buluu, usalama wa bahari, sekta ya usafiri na maendeleo endelevu.
Aidha,pamoja na masuala mengine, Rais Samia anatarajiwa kuzungumza na Watanzania waishio nchini Ufaransa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news