Fainali ya Mathayo Cup 2022 kwa watumishi wa umma kupigwa Jumapili

NA FRESHA KINASA

MBUNGE wa Jimbo la Musoma Mjini mkoani Mara, Mheshimiwa Vedastus Mathayo Manyinyi anatarajia kuhitimisha mashindano ya Mathayo Cup 2022 kwa watumishi wa Serikali na mashirika ya umma siku ya Jumapili ya Aprili 3, 2022 katika Uwanja wa Posta uliopo Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara.
Kabla ya fainali kufanyika, kutakuwa na mechi ya kutafuta mshindi wa tatu ambayo itaanza saa 02:00 mchana kati ya MRRH V/S TTCL ambapo itapigwa katika uwanja huo na kushuhudiwa na wananchi wa Manispaa ya Musoma pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi.

Aidha, pambano la fainali litawakutanisha Kati ya RAS-MARA V/S MASHTAKA (NPS) majira ya saa 04:00 za jioni hadi saa 06:00 jioni ambapo Mheshimiwa Mbunge Vedastus Mathayo Manyinyi atashuhudia mchezo huo akiwa ameambatana na Waheshimiwa madiwani wa Manispaa ya Musoma.
Wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini na Mkoa wa Mara kwa ujumla wameombwa kujitokeza kwa wingi siku hiyo, kwani michezo ni furaha, amani, ajira na pia ni fursa ya ajira na kuimarisha afya sambamba na kudumisha mahusiano mema katika jamii na Taifa pia.
Nao wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini wakizungumza na DIRAMAKINI Blog, wamempongeza Mbunge Mheshimiwa Vedastus Mathayo kwa kuendelea kushirikiana na wananchi kwa kuwa karibu katika kuhakikisha gurudumu la maendeleo linasonga mbele kama ambavyo aliwaahidi kuwatumikia kwa moyo wa dhati.

"Mheshimiwa Mathayo amekuwa akishirikiana na wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini wakati wote, amekuwa akifanya ziara za kutembelea kila mtaa na kata kusikiliza changamoto na kuzipatia ufumbuzi papo kwa hapo.
"Pia tumeona akifadhili mashindano mbalimbali ya michezo kwa vijana na kuwapa zawadi washindi, hii ni hatua njema katika kukuza vipaji kwa vijana na kuimarisha mahusiano mema baina ya vijana na kuwafanya wathamini michezo huyu ni kiongozi bora ambaye Mungu ametujalia. Mungu azidi kumpa afya njema,"amesema Ester Peter mkazi wa Kitaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news